Africa Kids Book Club

NDOTO NILIYOKUWA NAYO

 

Nilipokuwa mtoto, nilitamani kuenda Mombasa. Usiku moja,nilikuwa na ndoto. Kwa ndoto hiyo nilikuwa melini na ilikuwa ikienda Mombasa. Mama mrembo alikuja na alinipa kitu cha kula na kunywa. Tulipofika Mombasa,nilitoka Kwa meli,nilipata rafiki yangu huko Mombasa. Aliitwa Erica. Tulingia kwa gari na kupelekwa kwa hoteli. Tulipofika hotelini,tuliweka vitu vyetu chini na kuelekea kuoga baharini. Tulicheza Kwa maji hadi machweo. Tulitoka baharini na kurudi hotelini.

Sisi tulienda kutafuta wanyama. Tuliona wanyama wengi kama Simba, Tembo na Mbwa mwitu. Tulikimbia tulipomuona simba naye akatufuata. Askari alikuja na kumchukua simba na kumrudisha porini.

Usiku ulipofika nilioga halafu tukaenda kukula chakula. Tulipomaliza kula, tulipiga mswaki nakutazama televisheni. 

Niliamka na kumweleza mama kuhusu ndoto yangu.


Zoey Imende (9yrs) 

Mwanafunzi  kutoka kaunti  la Nairobi.

Januari .25 . 2025 

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *